ASKOFU MTEULE ROBERT PANGANI KMT JKM KUSIMIKWA RASMI JUNI 2,2024

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 16 апр 2024
  • Ibada ya Mbaraka kwa Askofu Mteule Robert Pangani wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi itafanyika Juni 2,2024 Viwanja vya Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji Jijini Mbeya.
    Akitoa taarifa kwa Wanahabari Makamu Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania Askofu Kenani Panja amesema mgeni Rasmi katika hafla hiyo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.
    Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Israel Mwakilasa amesema mbali ya Rais wageni mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wamealikwa kuhudhuria hafla hiyo.
    Askofu Mteule Robert Pangani atakuwa Askofu wa tatu kushika nafasi hiyo baada ya watangulizi Askofu Yohana Wavenza na Askofu Alinikisa Cheyo.

Комментарии • 2