Mtangazaji wa runinga ya Citizen Lulu Hassan atuzwa mjini Dar es Salaam

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 11 сен 2024
  • Mtangazaji wa runinga ya Citizen Lulu Hassan ametuzwa kwa mchango wake katika kukuza talanta kwenye fani ya filamu Afrika Mashariki
    Lulu aliyetuzwa kuwa mwanamke jasiri na mwenye bidii alipokezwa tuzo hilo kwa jina "Mwanamke wa Shoka" Afrika mashariki kwenye hafla iliyoandaliwa mjini Dar Es Salaam Tanzania. Wanawake wengine waliopokea tuzo hili ni pamoja na msanii wa Tanzania Lady Jay Dee. Lulu ametambuliwa kutokana na mchango wake katika kuhakikisha fani ya uigizaji inajumuisha talanta kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika Mashariki ikiwemo Kenya na Tanzania. Miongoni mwa Tamthilia ziizochangia tuzo la Lulu ni vipindi vya sasa vya 'KOVU' na SULTANA vinavyopeperushwa kwenye runinga ya Citizen na Maisha Magic pamoja na vile vinavyopeperushwa Tanzania vikiwemo 'HUBA' na MIZANI YA USHAMBENGA. Vipindi vingine vilivyochangia sifa na tuzo ni vipindi maarufu vya Maria, Zora, Maza, Aziza na Moyo ambavyo vilipeperushwa hapa kwenye Runinga ya Citizen. Heko kwa Lulu ni kikundi kizima cha Jiffy Pictures kwa ushirikiano na Big One Entertainment. waandalizi wa tuzo hizo ni stesheni ya radio ya E- FM na TV- E za Tanzania.

Комментарии • 29