Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
HTML-код
- Опубликовано: 15 сен 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Ukiitoa show ya ruge kwenye mkasi, hii ndo show bora ya salama, mahojiano yenye contents. Nime enjoy na kujifunza big up y'all
Masoudy ni kama muda wake ulikuwa mdogo ilifaa aendelee kutuambia mambo mengi zaidiiii ....... nimejifunza I wish maisha plus irudi tena
This is the one of the Greatest Man in the World, pengine hatukumwaga damu back in a days kipindi cha uhuru, ama pengine amani tuliyonayo inatufanya tunarelax na kujisahau but INAWEZEKANA
indeed
Hilo swali la "Tanzania yako unaiona wapi" majibu yake aiseeee, ni akili ya kiwango Cha juu Sana🙏🙏🙏🙌
Salama J! Kipindi chako kinaelimisha, kinajenga ujasiri, kinakuza kiimani. Nawe Mungu akuweke kama ulivyomwambia Masoud
Hakika nimejifunza vitu vingi na ninazidi kujifunza 🤲🙏salama 🤲🙏masoudy🤲🙏asantee kwa darasa
This guy is one of a kind my best quote "mnanunua hela mnapata wapi" kama nyie ni consumers na si producers
Kali sana hii na nilikua naisubiri hongera kwa kutuletea huyu mtu, sasa bado SALAMA NA MILLARD AYO
Salama kama unahitaji kujua uwekezaji was hisa na Hati fungani niambie. Ntakusaidia elimu for free. I am your fan
Kaka John .naomba uniongeza na mimi
Namm nahtaj weka no bro
Mimi nataka kujua pia
Nakupenda sana Masoud, huwa sichoki kukusiliza. MUNGU azidi kukutunza, una vitu vingi sana kwa ajili ya kuisadia jamii yetu (nchi yetu). Salama, nakupenda pia, kipindi chako kina mambo mengi sana ya muhimu kwetu. Big up you all!
Watu wasikujue saana...Familiarity breeds contempt Masoud nailed that
Mtu muhimu sana kwenye taifa letu na maisha ya WaTanzania ...💯🔥
Yani intrerview imeisha wakati ndokwanza inataka kuanza
Mungu akupe umri mrefu na Afya NJEMA Masoud Wetu 🙏
Strong heart Boss Kipanya, hiyo mentality wachache sana wanazo hasa wababa so tumejifunza mamb mengi sana hapo hasa sisi wanaume…be blessed Salama zaidi tupe watu makini sio wale channel za udaku na kutafuta umbea😂😂
Nilikuwa nampenda malkom tangu akiwa mdogo japo nilikuja kumuona akiwa amekuwa kuwa,nakumbuka nilikuwa ndo kabinti niliuwa sipitwi na kipindi cha wàtoto chuchuchu , kaka masood na malkom,marehem Amina chifupa na rahmani,,yaani nino, na kaka bonda yey hakuwa na mototo walikuwa wakimcheka kimatani,,aisee
Kipindi kizuri...shukran kwa Mtangazaji,shukran kwa mgeni Ustadh Msoud...tumenufaika na kufaidika piya kupitiya mazungumzo yenu...
God bless you masoud wewe ni genius sana aise naamn watu walio karibu na wewe kuna vitu vingi sana wanavipata kutoka kwako ,pia nikupongeze sana salamaa uko smart kwenye kazi yako #greatinterview
Masud kipanya ni Kati ya watu wenye fikra nyingi sana katika nchi ya Tanzania na bara lake sema sisi watu weusi tumeloga na aliyetuloga kafa, watu Kama yeye uwa tunawachukulia kawaida sana …… mungu ampe maisha marefu kaka yetu kwani bado ana mambo mengi sana kutujuza toka kwenye kichwa chake, Salama sina mengi ya kusema juu yako , you one of the best interview ever live in our generation, was good talk I love it
What an Interview.....Absolutely Sensational!
Shukran sana Kwa hichi Sister Salama,mbalikiwe sana na muishi sana
Masoud Amezaliwa Zama Ambazo Sio Zake,
Atusamehe Bure,
Tukitaka Kumuelewa Tumpe Nchi.
Masoud I'm 55years, I studied mechanical engineering, based to motor vehicle, for over 30year, you inspires me big time, man you have great mind weather we want it or not but the truth stand still,
Is there any chance we can meet, I would say we are some way alike, I'm a practically man ,you won't regret lay the table with me,
Plz Salama tuna muitaji tena japo 2hrs tu maana Ana vingi vya kutufunza
From Kansas in USA 🤜🏿🤛🏿
Niliona kama kuna mengi tunahitaji kujifunza toka kwake
Vp ile show ya maisha plus bonge moja la show itufunza mambo mengi sana kama vijana tunaihitaji tafafhali
Great interview. Thought-provoking. Masoud has a big mind.
Kuna content mmezikata na zilikuwa zinaumuhimu mno sanjari na Hilo bado show ni Kali mashaallah
There is very thin line between love and hate🔥
Duuuuhhh!! Nimejifunza kitu kikubwa saaana, hongera sana cis Salama na big up kaka Masoud, Mungu aendelee kukuweka na kile kilichopo ndani kiendelee kumea
Huwa sikuzote simalizi kiu yangu ya kumsikiliza Masoud, nimeangalia interview zake nyingi sana lakini bado nataka zaidi na zidi.
Daaaaah nimejifunza kitu kikubwa Sana thank brother 🙏
salama si haki hii ya mwaka jana iruduwe bwana
Men 🎉 Big up to Masoud I like your critical thoughts. Asante salama
Safi sana Masoud.
Hapo kwenye Business Plan. Ni Ukweli Mchungu. very true.
This is the best asante sana salama 🙏
Masoud, my faviurite presenter…since Chuchuchu ya Clouds fm, power breakfast…you are genius
Hiii show imekuwa fupi sana. "Tafuta taarifa upate maarifa"
❤ masoud, thanks Salama but please mrudishe tena tafadhali 🙏🇹🇿🇨🇭
Hakika nimejifunza kitu kwa brother masoud,Mimi nataka kitabu nitakipata wapi?
Rais Anateua Watu Kushika Nyadhifa MbaliMbali Katika Serikal Na Maeneo Ya Nchi Lkn Iman Yngu Mpka Leo Bado Hajajua Ww Utashka Nafas Gani Ww Ni GENIUS
Naomba umuhoji Masoud kila siku...
🤣
I have worked for 30 years I did different kind of innovation, at the meantime I'm thinking of working with sustainable agriculture based to irritation, your a philosopher,
SHIRT LAKE KALI SANA
Let me challenge Masoud, Dubai leo ina mafuta na utalii hela wanapata huko as Nation, Urussi ina Gas na Mafuta inapata fedha hapo, sisi tuna Gas, Madini, Utalii how we optimise these resources ziwe na tija kwa Taifa huoni kuna sehemu hatuko sawa, our Gvt needs to be Rich enough tukifika hapo itakuwa simple wao kufacilitate hizo manufacturing ma exports na kuleta Technology mpya, Serikali kama hela ya budget yake ni mpaka itafutane hatufiki, hiyo china, Marekani, Urussi, hata urabuni serikali zao zina hela nyingi sana kwakuwa ni wakali na wamesimamia ukweli kwenye resources zao!!
Shida kuu Kwa nchi zetu ni ,
Elimu na ufahamu,
Tumekosa elimu na ufahamu Kwa viongozi,mtu mmoja mmoja na jamii zetu,
Hizo nchi uzitajazo Zina technology, knowledge,
Ufahamu huo huwapa ,
Mawazo, ambayo huwatafuta watu sahihi Kisha hao watu huwapa mtaji / capital ambayo huleta kutatua changamoto za kidunia Kisha hupata zawadi( fedha nyingi/ THAMANI zaidi.
Kwa hiyo Kuna haja kubwa ya kuwekeza kwenye wazo ( maarifa)Kisha technology ( mifumo ya uzalishaji Mali kisasa ,na ndipo tufike mbali ,HUKU TUKIJUA UJASUSI WA KIUCHUMI KIMATAIFA .
Bado sana
NAWAKUBALI SANA.NBRO.masoud Kipanya nakukubali sana
This is hands down the best interview I have listened to tangu hii show ianze
Masoud amebarikiwa IQ kubwa..! Best Interview 🙏
Hawa ndo watu wa kuwekwa serikalini walete elimu na mabadiliko katika jamii, siyo tuu watu watuuu
Masoud akili nyingi sana.. very inspired
Hili ni darasa huru nimechukua point za kutosha sana leo, ahsante.
Yaani baba Malcolm iko kama Mimi simtu wamarafiki.naninapenda saaaana kuka pekeangu kwa sababu Mimi nafkiria saaaaaaaana
Super genius🔥
masoud anaongea vizuri na kwa ufasaha sana
hua namuelewa sana huyu jamaa. (kipanya) ni moja ya hazina , well done , please tuletee kaimu shehe wa mkoa DSM.
Genius Masoud.
I love Masoud Kipanya huyu jamaa ana akili nyingi sana
Nimependa hapo kwa rafiki
Akili hzi za masoud Hawa ndio ilitakiwa wawepo bungeni,bahati mbaya wapo Africa.
12:10,🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌, magari siyo matikiti au siyooo😂😂
Big brother is not a show to impact an African community, nothing in there.
May Allah make it easy for Kipanya to continue with MaishaPlus
Ruge Mutahaba, Masoud kipanya ,Massanja,Zembela, Roma mkatoli ,Nauka nafikiri Hawa jamaa Tanzania inabidi iwatumie sana!
Salma na ston town show naomba mniruhusu nitukane ili kiongozii wetu ajee hapa kumsikiliza huyu Kaka 😢😭😭😭
Big up brother Masoud na dada yetu Salama
only content in this mahojiano 🎉
Bonge la interview 👏👏👏
Duuh bonge la interview
Voice over artist
Nakukubali kaka
Makini broo❤❤
Nimejifunza shukran sana kwenu
On Podcast is 2 good hours, this is summarized.
Masud nakukubali na kunakitu chakujifunza toka kwako
Masoud mtu special
Ningefurahi sana Kama nitapata namba ya Kipanya, from Germany
Big brains maahn🙏
Nasubiria salama na Roma mkatoliki, salama na Kala Jeremiah
Asaalaam Alleykum naomba utuletee na ezden jumanne!
kitabu chake kinaitwaje na kinapatikana wapi
Maisha plus ingerudi Tena
Hakika,
SISI WA TANZANIA NI WACHUUZI KABISA.
BIDHAA ILIOTENGENEZWA NA MWINGINE HALAFU UNANUNUA ILI KUUZA KWA FAIDA
12:13 utemgenezaji wa magari sio kilimo cha matikiti😉😉
Usimruhusu mtu akakujua kuna siku atakutumia vibaya sana kukujua kwako
Natamani sana kama utakuwa unaleta watu wahivi wengi kuliko ambao hawana uwezo mkubwa wa kuzungumza vitu sensitive kama hawa mkifanya hivi wallah mtafika mbali hata vipindi vyenu kuwa namba 1 tanzania kuliko channel nyingi za hovyo cause hapa kuna vitu vingi vya kujifunza
Mi napenda tu slama tabasam lake
Masoud kipanya atafutwe tena, bado hajakata kiu yetu kama watazamaji
Why wasimpee aat uongoziii uyu jamaaaa ... mee naaminii iii Dhahabu kwa watanzaniaa aseee
Moja kati ya watu ambao wanafanya nijivunie kua Mtanzania
Wakwanza
Jmn mahojiano mbn mafupi
wa pili
I wish Maisha plus Ingerud tena ngoja tuendelee kuomba dua
Watatu
Startup is hassling 🛺💪🏿, asante sana KP
eMo Bodaboda Tanzania