MFAHAMU KIJANA HUYU MTANZANIA KUTOKA KIGOMA ALIYEJIUNGA MAMELODI SUNDOUNS YA AFRIKA KUSINI

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • MFAHAMU KIJANA HUYU MTANZANIA KUTOKA KIGOMA ALIYEJIUNGA MAMELODI SUNDOUNS YA AFRIKA KUSINI
    Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amemtakia kila la heri kijana Malik Hussein Malik (17) kutoka mkoani Kigoma aliyekuwa akiichezea Timu ya Vijana ya Azam FC ambaye amefaulu katika majaribio na sasa anaelekea kujiunga na Timu ya Vijana ya Mamelodi Sundowns ya nchini Afrika ya Kusini.
    Akizungunza na waandishi wa habari ofisini kwake alipotembelewa na kijana huyo kwa lengo la kuagana, mkuu huyo wa mkoa amemsihi Malik kwenda kucheza mpira kama kazi badala ya kucheza mpira kwa kujiburudisha.
    "Huyu ni balozi mzuri kwa nchi yetu, pia atatoa hamasa kwa vijana wengine ambao kila siku hucheza mpira hadi kwenye maeneo yasiyo rasmi bila kujua kuwa wanachokifanya ni sehemu kubwa ya ajira inayoweza kuyabadilisha maisha yao iwapo watajiendeleza na kuamini katika vipaji walivyonavyo," amesema Andengenye.
    Malik amesema alifanya majaribio mwishoni mwa mwaka 2023 na anatakiwa kujiunga na timu ya vijana ya klabu hiyo.
    .
    .
    .
    .
    #trending #raissamia #ikulumawasiliano #ccm #mwanza #mwanza #daressalaam #ilemela #kigoma #mamelodisundowns #southafrica

Комментарии •