Aunty Asimulia Alivyokutana Na Kusah "Alinifuata DM, Alikuwa Anatafuta Chaka" | SALAMA NA AUNTY PT 2
HTML-код
- Опубликовано: 5 фев 2025
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Nikuibie tu siri ya kabatini kuhusu haya mazungumzo yangu na Aunty Ezekiel, kwanza ilikua ngumu sana mpaka alipofika hapa kwenye kiti maana mazungumzo haya yalighairishwa zaidi ya mara tatu mpaka ilipofika siku hii. Kwa imani yangu nisema Mungu ana mipango yake, yaani kila kitu kwa wakati wake na bila ya shaka wakati wa hii ulikua haijafika bado ndo maana haikutokea na kwa kutokea siku hii, huu ndo ulikua wakati sahihi kabisa.
Mimi na yeye tunafahamia ki vyetu, si watu ambao tunakutana kila siku ila ni watu ambao tukikutana tuna click tu vizuri na mambo yanaenda. Marafiki zetu wengi pia wanafahamiana kwahiyo tunaenda tu vizuri. Na nia na madhumuni ya sisi kumtaka kwenye kiti chetu ni kwasababu wote tunajua amepitia mengi na kwa yeye kutusimulia kuhusu makuzi yake na mahangaiko yake yanafaa nafasi kwenye kiti chetu.
Toka mara ya kwanza kusikia jina la Aunty Ezekiel naamini miaka mingi tu ishapita, kama wewe ni wale wa zamani kama mimi basi utakua unamjua toka miaka ya katikati ya 2000 baada ya kuwa mmoja ya kundi la wasichana wazuri ambao walishawahi kushiriki Miss Tanzania. Kwenye mwaka ambao Aunty alishiriki kulikua na warembo kama Wema Sepetu, Jokate Mwegelo na Irene Uwoya kuwataja tu wachache. Aunty yeye naye alikua kati ya wale waliongia Top 10. Mwaka huo ulikua mwaka wa ushindani sana lakini wengi ambao walimaliza vizuri ndio hawa mpaka leo wanaendelea kufanya vizuri katika nyanja mbali mbali ambazo wao wamezishagua.
Aunty sasa ni Mama wa watoto wawili ambao ameniambia ni kila kitu kwake, wanampa sababu ya kutaka kuendelea kuishi na kuwa bora kwao kila wakati, nilimuuliza siku ya kwanza alipompata mtoto wake wa kwanza, na hisia yake ilikuaje, na anakumbuka jinsi ambavyo aligundua ana ujauzito na mara ya kwanza anamshika Cookie mikononi mwake.
Aunty pia anakumbuka ‘ujana’ wake na mengi aloyapitia mpaka akawa hivi alivyo leo.
Kuna suala la yeye kuwa na mahusiano na wanaume ambao ni wadogo kuliko yeye, au wale ambao alikua nao zamani ambao walikua wakubwa kuliko yeye, Aunty amenielezea maoni yake juu ya hili. Mahusiano yake na Marehemu Mzee wake, Mama yake.. Alivyolelewa na machaguzi ambayo aliwahi kuyafanya wakati anakua na pengine maamuzi mabaya au kama ana majuto katika maisha yake.
Kama binadamu kuna baadhi ya mambo yanakua magumu kuwa nayo wazi au kuyaelezea kinaga ubaga, Ila hata kwa haya ambayo tuliongea nae natumai utapata ya kujifunza kupitia yeye.
Tafadhali Enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
A humble down to earth person na yuko muwazi haoni haya kusema yy hajasoma ilhali yy ni star!
Aibu gani wakati ndio uhalisia wa maisha yake
I admire the maturity in this woman.... More love from 254
Nimependa hii interview,coz aunty Yuko open and happy...pia mama la mama salama amecheka sana♨️♨️♨️
Weka like kama huja soma sana ila MAISHA yanaenda..
Yani wanawake wote wangekua km Unty wangefanikiwa sana, yani yupo free na maisha yake yupo open alafu hajali wala nini, yani Unty ✔️
Nimependa jinsi aunt alivyo open kwa kweli 🔥🔥🔥🔥🔥🔥
🤣🤣🤣 ukweli humuweka mtu huru hongera aunty kwa kuwa mkweli 👏👏👏
Wasanii underestimate how much we appreciate and enjoy their honesty.💯
Nimependa Sana hayo mazungumzo kwa sababu yanafundisha pia. Mimi natamani salama naye ahojiwe maana naye nipasua kichwa, na kama kungelikuwa na uwezekano ningeomba nimhoji mm mwenye 😃🥰
Beautiful conversation... Ningependa kumuona Iren pol please 😍
Batuli😂
Napenda sana maongezi yenu yanakuwa kama mko best friends
Any interview ya Auntie Ezekeli lazima nitazame sababu ni real sana. 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪
Napenda Aunty Mungu amupe maisha marefu hadi siku moja tu meet naye m niko Congo 🇨🇩
Nimekupenda sana jamani Dada ante umenitia moyo sana nisonge mbele Mimi ni MWIMBAJI NA MWIGIZAJI NINA ALBAMU YANGU NA FILAMU HAIJAISHA NIMEKWAMA NAITWA ENIZE MWAYINGA please naomba msaa wako nipe ushari nanionye njia na mimi Dada niko tayali kupambana
Salama naomba utuleteye sheikh Kishki nourdin , mtakuwa mmetisha sn , sio wasanii tu siku zote
Fili Gisi Kuku Mwehu Na Zigo La AY hii nimeipenda sana. By Salama on kipindi (HOT SEAT)
Oh man‼️ Have enjoyed this to the extent 👌
Asee nimecheka sana nyimbo ya ant na harakat za kuludaxubh love xana ant💖💖💖💖💖
Tuletee Aliyah wa wasafi(refresh),nahisi interview yake itakua so inspiring
Hongereni salama,tunamuhitaji wema naye aje kwenye intaviu
So hilarious 🤣🤣🤣🤣 Uliimba Watanzania hawakukubali😍😍😍 LOL 😆
Salama support kubwa kutoka kwangu....watching from dubai Kila session nawatch ila tunamuitaj Mr blue AKA kabaisa muhimu ni kujifunza kutokea kwenu
Dada salama, Nakuomba utuletee Kondeboy mezani. Tunaomba kusoma kutokana na ujasiri wake
Was a nice interview 👌 👍 aunt she's very really 👌
Shes so pure i realy admare you Aunty..love you mama of 2 and still cute
Much love from 254
My dear ww nimtu wang wa damu kbs #AuntyEzekiel nakupenda mpaka naumwa kweli ❤❤❤❤❤
Ant wewe ni mrembo sana na umebarkiwa vingi sana❤️
Napenda anavo support masomo na mtoto wa kike asome
Nimependa aunt ❤anaongea vizuri pia yupo wazi sana
INTERVIEW TAMU HII NATAMANI ISIISHE AUNTY NIMEPENDA SANA THE WAY ULIVYO
Mahojiano mazuri sana na aunt amekuwa muwazi.. Nimeipenda,
Naomba nimkosoe kidogo aunt
Sema una friends lkn hauna best friend... Ndio maana friends Zako wana akaunti fake... Highligh point ni hapo kwenye Msosi filigisi mwehu na zigo la AY.. hahahaaaa... Hapo sijaielewa hiyo menyu... Salama tunaomba ufafanuzi plz
Hongera sana anti nimependa unavyoongea lugha moja2 sio wale wanaochanganya changanya
Ningependa kumuona Mchungaji Hananja Rich bilinear 🙏😂
Interview nzuri Inachekesha Kimtindo
Ilove mama cookie ,, how honest she is big up salama
Aunty nampenda hapindishi maneno😂😂
Sana
Kiwanda cha maarifa namkubali sana salama jabir anajua kweli kweli
Nimenjoy hii interview sanaaaaa.Da salama natamani siku aje Dina Marious
Her honesty 🔥
NMESIKILIZA NYIMBO YAO SAIV NMECHEKA SANA ILA CJAJUA KAMA KWAYA AMA BONGO FLEVA MTUHAJUI KUIMBA UYO JAMANI DAAAAAAH
🤣🤣🤣🤣 amenchekesha Aunty kwenye kuimbaa Lol!
Safi sana na hongera sana
Nimependa sana salama na mama nini🥰🥰🥰🔥🔥🔥🔥
Hakika yuko vizuri
Ni mama nono siyo nini
Icho chakula nimekipenda jina lake filigisi, kuku mwehu na zigo la AY 😂😂😂😂 ila ningependa aje diamond kwenye interview tuna mengi ya kumuuliza
Ant anaonekana n mtu mwenye akl sana, ata kama apendi mambo ya uongoz ila m nahs anafaa tu kuwa kiongoz, napenda confidence ya ant alafu yuko very straight
Awe kiongozi wa nini Mamy,
Napenda Irene uwoya aje pia kwenye meza hiyo plz salama fanya hivyo
next time tunamtaka jennifer mgendi muimbaji wa injili please
Aunty Mrembo Mashallah
don't quite understand this food bit - doesn't the food get cold? but good conversation. keep it up.
Best Interview ever
Aunty ni mzuri nyie mashallah
Sanaa
Nikweli anty nimzuri
Appreciate.!
Was really waiting for this interview I love Aunty Ezekiel
So humble
Nampenda Aunt Ezekiel, mkweli sana.
🤣🤣🤣anasema yeye na shule No😂😂Aunty wewe
Mansha Allah ATIunatup ushaur mzur saan
Aunt umenifurahisha Sana unasema ukweli kabisa
Mbona vidole viwili havina kucha
Nimeipenda. Nzurisana
🤣🤣🤣 Aunty Bwana Msema Ukweli Hadi Rahaaaa
Bongo movie "mlijipoteza" kwa kung'ang'ania kuiga movie za Africa Magharibi kuliko kuigiza vya kwenu Tanzania... Kama walivyo jitokomeza muziki wa dansi kwa kujipendekeza kuiga muziki wa Congo\Zaire.
Aunt Ezekiel nimependa your honest
Hii nimeipenda sana
hakuna shida ila haikuwa kipaji chako bwana sio lazima wote tutoke kupitia elimu
Ila ant nakupenda sana jmn🤣🤣🤣🤣🤣
Hi salama am zamda wa kikwajuni Zanzibar naomba tuletee Mr blue
Aunt nakupenda sanaa 😊
Mama bora Aunt Ezekiel ulionekana kwenye move ya wewe na watoto wa Wema Sepetu ambao uliwabadilisha kitabia.
uko very smart
Ndio kyrat anajieleza vizur .nakumbuka miss bongo ilivuma na ndo ilimtowa
Hata mm yan mm na shule paka na pany 😂😂😂
Nakupenda saaaaaaaaaaanaaaa aunt
Ndio ni kwel mimi mwenyewe sipendi uongozi kwasababu iyo napenda uongozi lakin unakuwa haupo uhuru
Aunty mbn km upo vzr kwenye maswala ya kusoma ila haujikubali, I believe una akili sana ni vile tu haukuwa tayari labda kwenye mambo hayo
Aunty una Rudi lini kwenye tamthilia ya Huba we miss you3
I for one, think cougars with relatively reliable source of income love cubs because they want domineering over the poor boys, they want to live their life unchecked,unquestioned in whatever way, they want to be by themselves.In this relationship you will find unending bickerings and the cub being told off all the time.The cubs love dating cougars because they love being pampered like a mother pampers her kid and because they have unreliable incomes , they like sponging on their older women.There is no responsible love been two people who are intellectually and mentally far apart from one onether, age and mental capacity go hand in hand with age. Secondly a cougar who loves cubs cannot cope with mature and responsible reasonings of an older man, (a sign of arrogance, unmanageability, and strong headedness of a woman who cant cope with a mature man).The stark fact that God took sometime to create Eve after Adam explains why there should an age gap beween a woman and a man in their matrimonial union. Don't be swept away by these satanic and demonic stereo types that love ain't age or age is just numbers, only nerds and unrespectful of God's plan will always go anticlowise God's plan!Don't you ever be gulliable believing this nonsense. YOU heard,!! Peace out
Kazi nzuri sana
Mimi naijuwa iyo nyimbo nimbaya sana
Wameona na wao wacheze tamthilia kwasababu wakolea walishawapita bila hivyo
Ndio kuimba walisema hawezi .Mimi napenda kuimba na najuwa kaka yangu naye anajuwa anatunga pia
Big 5 yooo✌
Interview nzuri sana.. Lakini mimi kama mimi naomba muzingatie viti haviko kwenye muonekano mzuri vile.
Hivo wameweka kusudi hata meza
Ni makusudi😆😆😆
Mambo ya natural 😃
Hvy ni vzr mbn, wamepaka rangi km ya ovyo ovyo ila ndo style hy
@@khadijahali4837kusudi limekamilika hapo, labda kama utataka kuuliza ina maana gani sanaa ya kiti cha namna ile (maana kwenye sanaa kuna mambo mengi)
Ant muwazi sna ♥️♥️♥️
Yani leo mda wangu wamapunziko nimemsikiliza anti ni vile nampenda na hujutii ukimsikiliza mama kuku
😂😂😂asante kwa kuwa mkwel dada gwantwa
Kasema alikuwa anapenda nyimbo zake alisema kusah kuwa aliimbaga nyimbo yake.wengi hawakujuwa kama walikutana instragram walijuwa labda walionana live
Last time wema sepetu tunamhitaji ktk meza yako salama
Auntie hana Mambo mengi Yuko wazi!afu salama icho kiti ulichokalia mmmh ukipige rangi bana location mzr kiti chako mmmh nakukumbusha tu naona umejisahau
Nahisi ndio design.na Iko poa tu.samakisamaki kama unapajua ndio staili zake.
Kwel hakuwai kuwaza naona hakuamin alivyofuatwa DM
Nampendaka saaaana saaana anakuwaka mkweli
Kwny mambo ya shule shule nmecheka 🤣🤣🤣
Kipindi kikali sana ushafanya mambo nengi sana tuna mtaka mume wakoo umulete kwenye Interview please
Kasoma shule ya bunge watto wa wakubwa wengi walisoma shule ya bunge
Ndio tulifurah kwasababu hatujawai kuongozwa na mwanamke
Nimependa kiti cha da Salama
Jamani Aunty asiogope kufanya mambo kwa uoga, au kwakuhofia elimu yake. Mbona wapo wala saba wanaakili kuliko hao mnaohisi niwasomi? Wangine wanaelimu ya kukariri tu. Jaribu mambo bibie
Salama Diamond awe next hapo plz fanya @ big fans
Hamjui nyimbo ya aunt 😂😂😂😂😂😂
Kipindi safi sana.