KILIMO CHA MBOGA MBOGA AINA YA CHINESE(CHAINIZI).Vijana tujikomboe kwa kulima mboga inalipa

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 29 сен 2024
  • KILIMO BORA CHA CHINESE
    August 3, 2018 IBRAHIM
    KILIMO BORA CHA CHINESE : Spinachi ni moja kati ya mazao ya mbogamboga inayo limwa sana nchini Tanzania na asili yake ni china na ndo maaana huwa tunaiita chinese na badae likasambaa katika nchi mbalimbali ikiwemo na Tanzania.
    Mboga hii huwa haina msimu, hivyo mkulima anaweza kulima muda wowote ambao anataka, na hii itategemea upatikanaji wa maji wa maji kwa wingi. Kwani mboga hii huhitaji maji kwa wingi katika hatua za awali.
    kilimo cha mchicha
    kilimo cha chinese jamii forum
    kilimo cha mbogamboga pdf
    kilimo cha mbogamboga nyumbani
    ukulima wa mboga
    tajirika na kilimo cha mchicha
    kilimo cha mchicha wa kienyeji
    chainizi mboga
    HALI YA HEWA INAOYOFAA KWA KILIMO HIKI NI :
    Jotolidi : Chinese au Spinachi linastawi na kukua vizuri kwenye maeneo yenye jotolidi 18 °c hadi 27° c.
    Unyevunyevu : Chinese ni zao linalo tegemea umwagiliaji kama ambavyo nimekwisha eleza hapo awali hivyo linaitaji maji mengi wakati wa ukuaji.
    Udongo : Chinese cabbage linakua vizuri kwenye udongo wa kichanga na wenye unyevunyevu wa kutosha PH; 5.5 hadi 7.6
    KILIMO BORA CHA CHINESE
    KILIMO BORA CHA CHINESE
    NAMNA YA KUANDAA SHAMBA
    Udongo unatakiwa utifuliwe vizuri kabla ya kupanda unaweza kutumia jembe la mkono au machaku na chisel na andaa shamba wiki 6 kabla ya kupanda.
    UANDAAJI WA KITALU
    Kitalu kinatakiwa kiwe na upana wa mita 1 yani sentimita 100 na urefu wa mita 5 yani sentimita 500. Kitalu kitifuliwe vizuri na kiwe na kingo ili kuzuia maji kutoka nje ya kitalu. Kisha panda mbegu kwenye kitalu kwa sm 15 hadi 20 mstari hadi msitari na panda mbegu sm 2 kati ya mbegu na mbegu na fukia sm 1 hadi 2.
    KILIMO BORA CHA CHINESE
    NAMNA YA KUANDAA SHAMBA
    Udongo unatakiwa utifuliwe vizuri kabla ya kupanda unaweza kutumia jembe la mkono au machaku na chisel na andaa shamba wiki 6 kabla ya kupanda.
    UANDAAJI WA KITALU
    Kitalu kinatakiwa kiwe na upana wa mita 1 yani sentimita 100 na urefu wa mita 5 yani sentimita 500. Kitalu kitifuliwe vizuri na kiwe na kingo ili kuzuia maji kutoka nje ya kitalu. Kisha panda mbegu kwenye kitalu kwa sm 15 hadi 20 mstari hadi msitari na panda mbegu sm 2 kati ya mbegu na mbegu na fukia sm 1 hadi 2
    KUPANDA
    Kwa kupanda moja kwa moja chimba udongo sm 2 hadi 3 kwa kutumia jembe la mkono na panda nafasi ya 30 mstari hadi mstari na 30 mbegu hadi mbegu na fukia sm1 hadi 2.
    Na kwa kupandikiza hamisha miche inapo fikia urefu was sm 5 na chagua miche yenye afya na isiwe na magonjwa.
    MBOLEA
    Kama unatumia mbolea ya ng’ombe, kuku na nguruwe tumia ndoo katika kila kitalu chenye mita 5 na pia weka mbolea ya kukuzia UREA gram 50 kwa kila kitalu chenye mita 5 pale mmea unapofikia majani matano.
    PALIZI
    Tumia jembe la mkono kupalilia magugu pale yanapo jitokeza.
    MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
    Pale utakapohisi majani ya mboga hizi yameanza kubadikika, ikiwa ni ishara ya kushambuliwa na wadudu, tafadhari unashauriwa uweze kutumia kemikali za kuua wadudu kama vile ninja, supercorn, wilcron na perfecron na pia hakikisha kila wakati unakumbuka kuondoa magugu pamoja na mimea yenye wadudu na pia weka shamba safi wakati wote.
    Lakini kama utatokea ugonjwa wa Kuoza kwa mizizi unachotakiwa kufanya kuondoa mazao yaliyo athirika na ugonjwa huo.
    KUVUNA
    Chinese ukomaa baada ya miezi 2 hadi 4 inategemea na aina mbegu uliyopanda, au muda mwingine hutegemea na hali ya hewa pia.
    KUMBUKA
    Wakati wa kuvuna unang’oa kwa mkono au unaweza kutumia kisu kukata kuanzia chini kabisa ya shina ili kuruhusu majani mengine ya mboga kukomaa.

Комментарии • 14