RC MTANDA AMSAIDIA BIBI WA MIAKA 80 KUJENGEWA NYUMBA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 18 окт 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemuagiza Meneja wa Kiwanda cha Birchand Oil Mill kumtafutia na kumpatia Bibi Sophia Masunga mkazi wa Igoma Mwanza kiasi cha Tsh. Milioni 2.5 ili aweze kujenga nyumba na apate mahali pa kuishi kutokana na eneo lake kusemekana kuchukuliwa na kiwanda hicho tangu mwaka 1996.
    RC Mtanda ametoa maagizo hayo mapema leo wakati akiwa katika zoezi la kusikiliza na kutatua kero za wananchi Mkoani humo, ambapo amesema hakuna kumbukumbu yoyote ya kimaandishi inayomhalalisha Bibi Sophia kuwa lile eneo ka kiwanda ni lake hivyo amemtaka Meneja wa kiwanda hicho kutumia busara kwa kumpa pesa Bibi huyo ili aweze kujenga nyumba kwa kuwa eneo la kujengea analo.
    RC Mtanda amekuwa na agenda moja ya kukutana na wananchi wa makundi mbalimbali kila siku ya jumanne ofisini kwake ambapo amekua akisikiliza na kutatua kero, changamoto na kuzitolea ufafanuzi chini ya Wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi mbalimbali za serikali na binafsi.

Комментарии •