Wananchi 7000 walia na Rais Samia Handeni,wagoma kuhamishwa

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 3 окт 2024
  • Zaidi ya wananchi 7000 wa eneo la Bondo kata ya Kwamagome wilayani Handeni mkoani Tanga,wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan,kuwasaidia kutatua mgogoro wa mpaka wa muda mrefu kwenye eneo hilo,ambapo wanashindwa kufanya shughuli za kujiendeleza.
    Wakiongea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye eneo hilo kwaajili ya kusikiliza kero hiyo wakiwa na viongozi wa chama na serikali walisema,wapo hapo kwa zaidi ya miaka 40 na wamejenga miundombinu mbalimbali ila kwasasa wanatakiwa kuondoka ikielezwa ni hifadhi.

Комментарии • 4