Salama Na GARA B SE6 EP63 | BABA SHUGHULI PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
HTML-код
- Опубликовано: 16 апр 2023
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Jina MC Gara B ni miungoni mwa majina makubwa sana kwenye ulimwengu wa kazi ambayo mwenzetu huyu amechagua kuifanya. Familia yake, mke na watoto, wazazi wake na wa mkewe pengine, Ndugu jamaa na marafiki na waajiriwa wake wanakula vizuri kwasababu ya kipaji chake Ndugu yetu huyu. Ni mwanaume ambaye akiwa kazini kwake furaha na burudani ambayo huwapa wateja wake ndo inayomfanya azidi kuenda mbali kwenye tasnia hiyo ya ushereheshaji. Again, yeye ni mmoja ya BORA kadhaa ambao wanafanya kazi kama yake.
Mtandao wa kijamii ni kitu kimoja chenye nguvu sana kwenye miaka ya hivi karibuni, kwa ushahidi tulonao tushawaona wengi ‘wakitoboa’ kwasababu ya Instagram au sehemu nyengine. Mitandao iko mingi na kila mmoja na tobo lake la kufikia mjini. Kazi ambayo MC huyu huifanya yeye huenda na team yake kuiweka vizuri kisha ana post kwenye page yake yenye watu karibia MILIONI MOJA NA NUSU. Akizifikisha mjini kazi hizo wengi huvutiwa nazo na ambao wanakua wana shughuli nao bila ya shaka watamtafuta na kutaka kufanya nae kazi. Ubunifu wake ni wa kipekee kutokana na vingi na wengi ambao tumekua tukiwaona kwa miaka mingi sasa. Mtandao wa kijamii umemsaidia na unaendelea kumfanya awe bora zaidi ya jana.
Sasa, shughuli hii anayo ifanya ndo ambayo ilikua ndoto zake? Pengine alikua huku anamuona mtu fulani akiwa anaifanya hii kazi kwa ufanisi na ikamvutia? Ilikuaje mpaka akaingia huko? Kwa kumtizama haraka haraka tu utagundua Ndugu yetu ni MCHESHI, yeye anapenda kucheka na kuongea, ingawa hapo kwenye kuongea nako sio kiviiiile ila ni mtafutaji ambaye AMETIMIA. Story yake alotupa kwenye episode hii inajumuisha yeye kufanya kazi zaidi ya mbili kwenye kipindi flani hivi cha maisha yake ili aweze kuishi vizuri. Ki professional mwenzetu ni MWALIMU, ambaye hiyo kazi aliifanya hasa, na akaijumlisha na kazi ya huduma kwa wateja pale Tigo na wakati huo huo akawa anafanya kazi kwenye kiwanda kimoja hivi huko Pugu Road, hakua na wa kumdekea wala kumsubiria na hustle yake hiyo ndo ambayo anaenda nayo mpaka leo kwenye maisha yake.
Sasa kama Baba na mume kwa mkewe kipenzi ambaye naye alikutana nae sehemu ya kazi yake, Gara B ananijibu kuhusu uaminifu ambao anao kwa mkewe ambaye kwa mujibu wangu kama amekutana nae kwenye mazingira hayo, vipi hujiskia kila mara anapokua kazini mumewe ukichukulia huko ndipo walipo kutana na ndo ambapo wanawake wengi wazuri huwepo? Jibu lake lilikua na kuukonga moyo.
Alituhadhia pia kuhusu wazazi wake na jinsi ambayo ameweza kujitengenezea jina, siku ya kwanza alipopata kimeo cha ku host harusi ya watu ambayo kwa mujibu wake aliibembeleza sana na hakua amepewa nafasi, ila nafasi ilipojileta akanyoosha kwa umbali mrefu mpaka mengine yamebaki story tu. Na hii ndo ilikua simulizi yangu bora kabisa kuhusu kupata nafasi na kuzitumia vyema.
Yangu matumaini utaskiliza na kuangalia kwa makini maana humu anatupa simulizi zote za kutokata tamaa na jinsi ya kuchukua nafasi, ila pia anatuhadithia baadhi ya mitihani ambayo huja na umaarufu pia na jinsi ya kupambana nayo. Mimi nili enjoy na natumai itakua hivyo kwako pia.
Happy Holidays.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
RUclips Link bit.ly/RUclipsSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz - Развлечения
Salama yani katika kipindi chako nimejifunza kuwa ilikutimiza ndoto kubwa yeyote mtu unayoiona ni lazima kujianda vzuri na kukubali kujifunza ili kufanya kiufasaha ile ndoto yako muda ukifika. ulikubali kufanya vipindi vya interview (Mkasi) and hata kuwa judge and now unafanya vzuri kazi yako. hii formula ni ya kuitumia kwenye maisha yangu. Best of luck Salama. Positive vibes
Namfaham mwanao Jensen,ukimkuta sasa anajitambulisha mi mtoto wa Gara b,anajiita Gara boy.
Salama unafanya kazi nzuri sana.
Dah nimesikitika sana na ile story! Aisee una mke na nusu❤❤
Brother hongera sana uzidi kubarikiwa, Salama dada wa taida... big up sana,
Nakupenda sana dada salama kwa kazi nzuri. Me nakuona wewe ni mtaalam wa mahojiano.
DADA WA TAIFA NA MC WA TAIFA..
Hongera sana garb
Dah
Pc yangu iko vizuri mbona kwa interviews nyingine vinaenda sawa warekebishe bhana hamtaki kuambiwa au mnataka comment zipi jaman?
Best mc in Tanzania wish you the best ❤
Nlikuwa interview nzurrr ❤❤
Waaaaah
There are diff. In filming with motion here. But the show its awesome❤🎉
brain on point
Gara B,nakukubali sana Bro
❤❤
Wa kwanza😊
🔥🔥🔥
what a character Gara b.....
😘🤩🤩🤩
Dada wa Taifa 😂😂🤣
Anko Michael wa Anitha 😁
Next mlete salama na Joseph kusaga @salama
Gara whaaaat 😅🔥 ila Mange hadi auwe watu na blood pressure 🤔🩸 💔
Kama na muona mange kimambi anakuja tz 😂😂
sauti na matamshi ya mdomoni hayaendi pamoja watu wa sound warekebishe hapo
Labda simu yako mkweche
Sorry nilkuwa xjaichek
@@viceboy7368 basi usiwe mwepesi wa kujibu kabla ya kuhakiki kisemwacho nia yangu ni njema tu si kuharibu coz personally kuna vitu najifunza kupitia some of interviews ila quality pia ni muhimu hata kama nahitaji kusikia tu bila kuangalia mdomo wa mtu
Kwel dada
Jamaa wa editing kuna mahali sauti na picha haziendani
Dah
♥️♥️♥️
Dah
Dah