Musukuma afunguka kuhusu kikokotoo, "tunakwenda kutengeneza taifa la watumishi wezi..."
HTML-код
- Опубликовано: 16 апр 2024
- Mbunge wa Geita Vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema kuwa ikiwa serikali haitasikiliza kilio cha watumishi kuhusu kikokotoo itatengeneza taifa la wezi.
Musukuma amesema hayo leo Jumatano Aprili 17,2024 wakati akichangia makadirio ya mpato na matumizi ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa mwaka 2024/25.
Pambaneni wabunge kuhusu kikokotoo kinatuumiza sana unganeni wote kwa pamoja bila kumsahau Esther Bulaya Big up sana.
Msukuma anafaa kuwa mtu wa Fashen anavaa vizuri sana
Wabunge waache unafiki inamaana kikokotoo hawakupitisha wenyewe wanaleta salakasi zao kisa tunakaribia uchaguzi mkuu
Munger aliyetetea kikokotoo aanze kukatwa kwenye posho yake ili aone kilivyo.NAMALIZIA KWA KUMWOMBEA ASIRUDI TENA BUNGENI
Kama kikokotoo kina nia njema. Kianze na wabunge na madiwani na rais
Si suala la kujadiliana ni kurudi Tu 50%, well done King Msukima
Wenye pesa walishakataa. Hv kweli 140 mln umpe mstaafu 45 mln?!! Itamsaidia nini. Wape pesa zao wakajenge majinba ya wapangaji
Nguvu nyingi zinatumika kupiga kelele za kikokotoo, hivi nani ni muasisi wa hicho kikokotoo? Wakati kinaanza na kuanza kutekelezwa ninyi mlikuwa wapi? Kina wahusu wafanyakazi je mliwashirikisha katika kukiasisi? Je na ninyi mnapomaliza miaka yenu huwa kinawahusu? Hili jambo linatia shaka kwamba linataka mtu apate sifa katika kuliondoa ili kujijengea umaarufu. Ni aibu kutengeneza tatizo na kulifanya mtaji.
Kwenye posho zao hakuna kikokotoo kingewagusa wasinge pitisha pesa wanakata kutoka kwenye mshahara wako muda wa kulipa mashariti kibao
KIKOKOTO Cha wasitaafu ni wizi Wa SERIKALI yetu ,,,
Huu ni uonevu kwa kwel ndo maana wizi hauwezi kuisha 30% hapana kwann umpangie mtu na wakati pesa ni zake basi kama shikika halina uwezo wa kulipa hakuna haja ya watumishi kukatwa nssf
Wabunge waache kuleta salakasi wasiwalaumu mawaziri kuhusu kikokotoo wajitathimin walichofanya
Huwa ninakukubali kwa uwazi ulionao bungeni.
Umenikuna mweshimiwa
Nimekuelewa Doct. wa akili
Msukuma yupo sahihi.serikali inawadhulumu wafanyakazi. Sijuwi kwanini Bi Mkubwa kwa Nini hachukui hatua ya kuwasaidia wafanyakazi? Au kwa sababu yeye Ni Rais,aliacha urais,atalipwa pesa nyingi? Hii itamletea shida kwenye kura.uchaguzi utakuwa mgumu kwa upande wa wafanyakazi.itaketa shida
Kwa kweli hoja ya kikokotoo linaumiza sana watumishi. Ni vema serikali itafakari upya ili watumishi wajisikie wapi huru na nchi yao