Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua waliohusika kifo cha Baraka

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 26 сен 2024
  • Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa Kagera, Yusuph Daniel amesisitiza kuwa jeshi halitasita kuwachukulia hatua waliohusika na kifo cha Baraka Lucas (20) ambaye mwili wake uliopolewa ziwani katika Kisiwa cha Goziba ukiwa unaelea majini.
    “Tunaendelea na uchuguzi kubaini chanzo cha mauaji ya Baraka, haijalishi hata kama ni mtumishi wetu au ni mwananchi, taratibu za kisheria zitazingatiwa ili achukuliwa hatua. Wananchi naomba wawe watulivu maana wanahisi kifo cha kijana huyo ameuawa,” amesema Kamanda Daniel.
    Mwili wa Baraka ulikutwa ziwani Jumatano Juni 12, 2024 katika Kisiwa cha Goziba ukielea wakati siku tatu kabla ya kifo chake alikuwa akishikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo cha Goziba baada ya kukamatwa kwenye doria saa saba usiku Juni 10, 2024.
    Paschal Ibrahim, mkazi wa Goziba na baba mdogo wa Baraka, amesema wao kama familia ya marehemu wanaitaji kujua kwa nini aliyepelekwa mahabusu anaonekana tena ziwani akiwa amekufa.

Комментарии • 6

  • @azzaalhabsi1505
    @azzaalhabsi1505 3 месяца назад

    Subhanallah. Bukoba yetu hiyo.

  • @TinahLamajo-xb9xe
    @TinahLamajo-xb9xe 3 месяца назад

    Haki itendeke jamani
    Hawa askari wamezoea sana.

  • @SamwelPaul-mp6mx
    @SamwelPaul-mp6mx 3 месяца назад

    Kwanini msiende kufanya upelelezi sehemu tukio lilipotokea mkapata tarifa zaidi kutoka kwa wananchi kuhusu tukio Hilo na kupata ushilikiano kutoka kwa wananchi wa sehemu husika nasheria zikachukuliwa haraka ili iwefunzo hata kwa wengine wenye kujihusisha na matukio ya namuna hiyo Tanzania ni sehemu ya amani matukio ya namuna hiii hayatakiwi kabisa ili kulinda amani ya nchi yetu

  • @Rahabu-i1d
    @Rahabu-i1d 3 месяца назад

    Haki itendeke mana wamezoea watu wengi wamepotea huyu Mareham ndo amewaumbua

  • @mwanamwendy9265
    @mwanamwendy9265 3 месяца назад

    Mungu tusaidie jamanii, sheria sheria jamanii, kitu kama kinajulikana kwa nn hatua zisichukuliwe, huo uchunguzi 😭😭😭😭

  • @Theojenes
    @Theojenes 2 месяца назад

    😂mmmm